• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Bilioni 20 zimetumika kulipa Madeni ya Walimu

Posted on: April 29th, 2017

Bilioni 20 zimetumika kulipa madeni ya Walimu.

Katika kuhakikisha kuwa sekta ya Elimu inaboreshwa na kuimarika  Serikali ina mkakati wa kuhakikisha kuwa changamoto za elimu zinashughulikiwa na  kumalizwa kabisa ikiwemo utatuzi wa malalamiko ya walimu hasa madeni wanayoidai Serikali.

Mpaka sasa  Serikali imelipa madeni ya walimu ambayo siyo ya mshahara kiasi cha Tsh. Bilioni 20 kuanzia mwezi Julai-April 2018 , na kwa upande wa madeni yahusuyo mishahara Wizara ya Utumishi bado wanashughulikia.

Hayo yamesemwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Dkt Leornad Akwilapo kwenye sherehe za ufungaji wa Juma la Elimu zilizofanyika kitaifa Wilayani Nanyumbu  Mkoani  Mtwara kuanzia tarehe 24-28 April 2018. na kuratibiwa na Shirika la Mtandao wa eLIMU tANZANIA (TEN MET)

Aidha Akwilapo amewataka Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Kuacha kuisema vibaya Serikali na kutetea walimu kuwa hawafundishi kwa kuwa  wanadai stahiki zao.

“CWT acheni udhaifu wa kusingizia walimu hawafundishi kwa sababu ya madeni wanayoidai Serikali kwani madeni yanaendelea kulipwa kupitia mpango wa P4R(Perfomance for result).”alisema Akwilapo.

Kwa upande mwingine Dr. Akwilapo amewataka wanafunzi nchini kusoma masomo ya sayansi ili kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu wa sayansi uliopo kwa sasa. Aliendelea kwa kusema kuwa ingawa Serikali imeajiri walimu 4000 wa sayansi mwaka huu, imeboresha  vyuo vya Ualimu 10 na walimu 5900 wamepelekwa vyuoni kupata mafunzo ya masomo ya sayansi ili kupunguza upungufu wa walimu wa sayansi hadi kufikia 2018 bado haijatosha kuondoa tatizo hilo nchini.

Wakati huohuo Akwilapo amewataka wazazi kuwekeza kwenye Elimu na kuiweka elimu kuwa kipaumbele,  kuwaachia watoto urithi wa elimu ili kuweza kumuandaa mtoto katika maisha yake ya baadae.

“Tunapaswa kuwekeza katika elimu, hakuna uwekezaji bora kama elimu, mali zote zinaweza kuteketea lakini sio elimu, waachieni watoto urithi wa elimu, elimu haiozi, Elimu ni tunu ambayo mtu hawezi kunyang’anywa.”alisema Akwilapo.

Aidha amewataka walimu kuimarisha usimamizi madhubuti wa ufundishaji na ujifunzaji mashuleni kwani shule za watu binafsi zinafanya vizuri kwa kuwa usimamizi wao ni mzuri na wanafuata kanuni na taratibu za usimamizi wa shule. Pamoja na hayo amewataka pia kuacha tabia ya kuendesha bodaboda badala yake walimu watambue kuwa wao ni ngazi imara ambayo wanafunzi wanapanda ili kufikia malengo yao hivyo wajitume.

Vile vile Katibu Mkuu huyo ametoa agizo kwa wadhibiti ubora wa shule,Viongozi wa elimu wa Wilaya, Viongozi wa siasa kujipanga na kuhakikisha mtoto anapokuwa shuleni anakuwa salama kiafya  ikiwemo mtoto huyo kutotumia  madawa ya kulevya.

Dr Akwilapo  ametoa wito kwa watu wote kuhakikisha   Mtoto haachwi nyuma, mtoto anapata elimu, hata mlemavu asiachwe apewe elimu kama kauli mbiu inavyosema 'Uwajibikaji wa pamoja kwa Elimu bora,jumuishi na endelevu'. Aidha amataka Viongozi kuweka mazingira ya shule kuwa rafiki kwa walimu na  Wanafunzi ili kuboresha miundombinu ya shule ikiwemo vyoo, madarasa n.k.

Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.