Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani yapata ugeni wa waheshimiwa madiwani ishiri na nne (24) wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru wakiwemo wataalamu wanne (4) wa Kilimo, Uchumi, Habari na Afisa Utumishi , kwa muda wa siku tatu (3), kuanzia tarehe 19/10/2017 hadi tarehe 21/10/2017 kwa lengo la kujifunza uendeshaji wa Halmashauri , Maendeleo na fursa mbalimbali zilizomo ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Beatrice Dominic akiongea na waheshimiwa na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya Mtwara Mikindani , kuhusu uendeshaji wa Halmashauri kwa kuzingatia kanuni, sheria na utawala bora na kutoa uzoefu wake juu ya ukusanyaji wa mapato ya ndani, Utoaji mikopo kwa akina mama na vijana na usimamizi wa miradi ya maendeleo.
Wataalamu wa vitengo mbalimbali wa Halmashauri ya manispaa ya Mtwara Mikindani wakitoa maelezo juu ya uzoefu wao wa namna wanavyotekeleza majukumu mbalimbali ya kikazi na kutoa uzoefu wao kwa waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Tunduru.
Waheshimiwa madiwani na wataalamu walitembelea kituo cha utafiti wa Kilimo Naliendele kwa lengo la Kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu kilimo, na kuona uzalishaji wa mbegu bora za korosho, Ufuta na Karanga na kuona kilimo ya umwagilia wa karanga na ufuta pamoja na kiwanda cha kuongeza thamani na kubangua zao la korosho na uzalishaji wa bidhaa zinazotokana na korosho kama vile cashew butter, Jam, Juisi n.k.
Ugeni huo ulitembelea Bandari ya Mtwara na kujifunza namna walivyojiandaa na msimu mpya wa mwaka huu wa korosho katika kuhakikisha korosho zote zinasafirishwa kupitia bandari ya Mtwara. Pia walipata nafasi ya kutembelea mradi wa Dampo ya kisasa iliyopo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani na kujifunza namna watakavyoweza kutekeleza mradi kama huo.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA TEHAMA - MANISPAA YA MTWARA MIKINDANI
Manispaa Mtwara-Mikindani
Anuani ya Posta: P. o. Box 92,
Simu ya mezani: 023-2333102
Simu ya mkononi:
Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz
Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.