• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Kampeni ya ''FURAHA YANGU" yawataka wanaume kupima Ukimwi

Posted on: August 16th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe Evod Mmanda August 16,2018 amezindua Kampeni ya kitaifa ya upimaji wa VVU ijulikanayo kama  “FURAHA YANGU” inayolenga kuhamasisha umma wa watanzania hususani wanaume  kujitokeza kwenye zoezi la upimaji wa hiyari wa   virusi vya UKIMWI na kuanza kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi kwa wale wote watakaogundulika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo.

Akiongea kwenye uzinduzi huo uliofanyika kwenye viwanja vya Mashujaa vilivyopo  Manispaa ya Mtwara-Mikindani Mmanda amesema kuwa pamoja na kuhamasisha wananchi wote lakini mkazo zaidi umewekwa kwa wanaume kwa kuwa takwimu zinaonesha kuwa wanaume wengi hawapendi kupima  badala yake wanaweka  utegemezi kwa wake zao.

Amesema kuwa kampeni hiyo inalenga kumuanzishia dawa aliyekutwa na VVU ili aweze kuishi kwa furaha bila ya kuwa na hofu na  kuepuka magonjwa nyemelezi kwa sababu kinachoua sio Ukimwi bali ni virusi vinavyopunguza kinga mwilini na  kupelekea mgonjwa kushambuliwa na magonjwa nyemelezi na mwili unakuwa jumba bovu hivyo mgonjwa anapotumia dawa anazuia uzalishaji wa virusi.

Aidha Mmanda ametoa rai kwa viongozi wote wa halmashauri  kuwa wanatakiwa kuifanya kampeni hiyo kwa miezi sita mfululizo na kuhakikisha kuwa kila mahali penye mkusanyiko wa watu wengi  shughuli za upimaji ziwe zinafanyika.

Pamoja na hayo pia ameagiza viongozi wa halmashauri kuhakikisha kuwa vitendanishi  na dawa za ARV zinakuwepo za kutosha kwenye vituo vyote vya kutolea huduma  na kuwataka wananchi wote kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la upimaji wa virusi vya Ukimwi na watakaobainika watumie  dawa bila kuacha kwa kufuata masharti waliyopewa na wataalamu ili dawa hizo ziweze kufanya kazi mwilini.

"kuna watu wanagundulika na virusi, wanaanzishiwa dawa na madaktari, wanageuka madaktari wanaaza kujipangia mfumo mwingine wa maisha tofauti na ule walioelekezwa na wataalamu, matokeo yake unakuta dawa hazikolei, hazikidhi yale mahitaji yanayotakiwa mwilini kwa hiyo malengo na matarajio ya kufubaza yanakuwa hayajakamilika"alisema Mmanda

Kwa upande wake Mratibu wa kudhibiti maambukizi ya virusi vya UKIMWI Mkoa wa Mtwara Dkt Makarious Moris amesema kuwa Msingi wa kampeni ya FURAHA YANGU ni kutoa huduma za kitabibu ,kitabia na kimfumo. Aidha Kamapeni hiyo  ina ushirikishwaji wa mtu mmoja mmoja  na jamii kwa ujumla katika harakati za kutokomeza maambukizi ya ukimwi.

Amewataja walengwa wanaoguswa na mradi huo kuwa ni pamoja na watu wote ambao hawajahi kupima virusi vya Ukimwi na wapo katika hatari ya kuambukizwa au kuambukiza, watu wanaoishi na walioathirika na UKIMWI, viongozi wa dini na kiserikali pamoja na watoa huduma katika vituo na jamii. Aidha Kamapeni hii inahusisha afua za kitabibu, kitabia, afua ya mfumo pamoja na huduma ya afya.

Afisa Mradi wa HIV na kifua kikuu kutoka taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation Mkoani Mtwara Dkt Rose Kaaya amesema kuwa mradi wa Kampeni ya FURAHA YANGU unatekelezwa na taasisi hiyo katika mikoa minne ya Tanzania bara ikiwemo Manyara, Tanga, Mtwara na Arusha. Aidha kwa Mkoa wa Mtwara mradi huu unatekelezwa katika halmashauri mbili za Manispaa ya Mtwara-Mikindani pamoja na halmashauri ya Mji Masasi na utafanyika kwa miaka mitatu.

Amesema kuwa Upimaji utafanyika katika ngazi ya jamii ukidhamiria  kuzifikia wilaya 8 na Kata 184 zilizopo katika Mikoa hiyo, aidha jumla ya  Kaya zisizopungua 281 zilizopo kwenye Kata  zinatarajiwa kufikiwa.

Kampeni hii ya kitaifa ya upimaji wa VVU kwa hiari ilizinduliwa rasmi Juni 19,2018 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Khasim Majaliwa kwenye viwanja vya Jamuhuri Mkoani Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hii ni “FURAHA YANGU PIMA, JITAMBUE, ISHI”. Pamoja na uzinduzi huo pia shughuli mbalimbali za upimaji wa maleria, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi,upimaji wa shinikizo la damu na sukari,utoaji wa damu salama,utolewaji wa elimu ya uchangiaji wa mfuko wa bima ya afya  iliyoboreshwa(CHF iliyoboreshwa) umefanyika.


Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.