• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Manispaa Mtwara-Mikindani Yapongewza Kwa Kutekeleza Vizuri TASAF

Posted on: December 31st, 2017

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu Mhe. George Huruma Mkuchika (wa kwanza kushoto) akipokea taarifa ya ujenzi wa nyumba ya Mganga Zahanati ya Lwelu


Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Utumishi na utawala bora Kaptain Mstaafu Mhe George Mkuchika amewapongeza Manispaa Mtwara-Mikindani kwa kuwa halmashauri inayoongoza kufanya vizuri katika utekelezaji wa miradi ya  TASAF ukilinganisha na halmashauri zingine zilizopo katika Mkoa huo.

Amesema kuwa kufanya vizuri kwa Manispaa hiyo kumetokana  na jitihada zilizofanywa na walengwa wenyewe wa kaya maskini pamoja na usimamizi mzuri unaofanywa na timu ya Wilaya pamoja na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Na hivyo kuzitaka halmashauri zingine za Mkoa huo kuiga Manispaa Mtwara-Mikindani.

Pongezi hizo zimetolewa disemba 30, 2017 na Mheshimiwa Waziri kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara alipokuwa anapokea taarifa utekelezaji wa shughuli za TASAF katika Mkoa wa Mtwara.

Baada ya kupokea taarifa hiyo Waziri Mkuchika amesema kuwa TASAF ni mpango uliobuniwa na Serikali katika kuondoa umaskini katika nchi hivyo ameagiza kuwa watu wote walioingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini kiujanja na hawakuwa na sifa kuondolewa kwenye mpango huo na kuhakikisha wanarudisha fedha zote walizozichukua.

Amesema kuwa lengo la Serikali ni kuifikisha TASAF kwenye vijiji vyote na kwamba hadi sasa asilmia 70 ya vijiji vimefikiwa na asilimia 30 iliyobaki itamaliziwa hivi karibu na  kuwataka Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya kusimamia mradi huu kwa kuhakikisha walengwa wanapata fedha kwa wakati, kuhakikisha wale wote waliopatiwa fedha kiujanja na hawakustahili fedha hizo zinarejeshwa na kuhakikisha fedha zilizotolewa zinatumika kwa wakati ili kosa la kurudisha fedha lisiweze kujirudia.

Aidha Mkuchika amewapongeza Walengwa wa Kijiji cha Rwelu kwa kuibua mradi wa ujenzi wa nyumba ya mganga iliyopelekea kutatua tatizo la kukosa lililokuwa linawakabili la kutopata huduma za afya kwa wakati kwa kuwa mganga alikuwa anaishi mjini (km 15), lakini kwa sasa huduma zote zinapatikana muda wowote kwa kuwa nyumba hiyo imesaidia mganga kuishi kijijini hapo pamoja na mkunga .

Pamoja na hayo Mkuchika amewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto shule na kuwataka kufuatilia Maendeleo ya watoto wao,amewataka kuhakikisha wanawanunulia wanafunzi sare za shule na kuwapatia chakula ili waweze kusoma vizuri na kufanya vizuri katika mitihani yao. Aidha amewataka wazazi na walezi hao kuhudhuria mikutano ya wazazi shuleni.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Byakanwa amezitaka halmashauri zilizofanya vizuri kwenye miradi ya TASAF zisibweteke ziendelee kufanya vizuri zaidi na kwamba maagizo yote aliyoyatoa Waziri yatatekelezwa. Amesema kuwa kuhusu walengwa kujiunga na Mfuko wa afya ya Jamii  MKoa umeamua kulifanya suala hilo la lazima na ameagiza fedha zitakazotolewa Januari walengwa wote ambao hawajajiunga kwenye CHF fedha zao zitakatwa na watakabidhiwa kadi  na kwamba ndani ya miezi miwili asilimia ya walengwa watakaojiunga kwenye CHF itaongezeka kwa zaidi ya asilima 90.

Awali akisoma taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Wa kunusuru Kaya Maskini Manispaa ,Mratibu wa Mpango huo bi Sylivia Mwananche amesema kuwa Jumla ya kaya 1328 zilitambuliwa  na kunufaika na mpango huo kuanzia March-April 2014. Na hadi sasa jumla ya kaya 1295 zimesalia baada ya zingine kuondolewa kutokana na sababu mbalimbali.

Amesema kuwa Jumla ya Tsh.  876,738,476.00 ya fedha zimehawilishwa kwa walengwa waliopo kwenye mpango kwa mitaa 36. Aidha kwa mwaka 2014/2015 na 2016/2017 Manispaa imetekeleza miradi ya ajira ya muda  kwa mitaa 35 ambayo imewezesha walengwa 1287 kujiongezea kipato na fedha jumla ya Tsh. 156,963,400.000 (2014/2015) na Tsh 148,862,900 kwa mwaka(2016/2017) zilihawilishwa.

Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.