• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Manispaa Yapongezwa kwa kununua Gunia 200 za Mahindi kwa ajili ya Uji shuleni

Posted on: August 13th, 2017

MANISPAA YAPONGEZWA KWA KUNUNUA GUNIA 200 ZA MAHINDI KWA AJILI YA  UJI SHULENI.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Halima Dendego ameupongeza uongozi wa Manispaa kwa kununua gunia 200 za mahindi na kukabidhi kwa walimu wakuu na wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari.kwa ajili ya kupika uji kwa Wanafunzi Shuleni.

Mahindi yaliyonunuliwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wa  mkoa ambapo aliitaka kila Halmashauri kutenga bajeti ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa chakula cha Wanafunzi.

Akizungumza kwenye zoezi la kukabidhi mahindi hayo lililofanyika Agost 12 kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ameipongeza Manispaa kutenga bajeti kwa ajili ya kuwapatia chakula wanafunzi shuleni, lakini pia kwa kutekeleza agizo la Serikali.

 Hata hivyo Dendego ametaka wazazi na walezi kwa kushirikiana na walimu wao kuona ni namna gani wanaweza  kufanya  ili watoto waweze kupata angalau mlo mmoja shuleni. Aidha amewataka kutambua kuwa jukumu la kumlisha mtoto shuleni ni la mzazi na walezi.

Awali akitoa taarifa ya zoezi la ununuzi wa mahindi hayo Mkurugenzi wa Manispaa Mtwara Mikindani Bi Beatrice Dominic alisema kuwa gunia 200 za mahindi  zilizonunuliwa ni awamu ya kwanza ya utekelezaji wa agizo la serikali na kwamba Manispaa imepanga kununua magunia 500 ya mahindi kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Amesema kuwa Manispaa imetoa mchango lakini wazazi wanatakiwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kusaidia Watoto wetu kupata mlo shuleni hivyo wazazi na walezi wawajibike kwa hilo.

Amendelea kusema kuwa  mahindi hayo yatagawiwa kwa shule za msingi 31 na sekondari 13 na kwamba ugawaji wa mahindi umezingatia idadi ya wanafunzi shuleni hivyo  kuna shule zitapata gunia 2 na zingine zitapata gunia 3. Hata hivyo ameahidi hadi kufikia mwishoni mwa robo ya kwanza 2017/2018 kila shule itakuwa imeshapata gunia 4 za mahindi.

Katika bajeti yake yake ya 2017/2018 Manispaa imetenga kiasi cha shilingi milioni 30 kwa ajili ya ununuzi wa mahindi ya uji wa Wanafunzi Shuleni na hadi sasa imetumia shilingi milioni 7,600,000 na kununua gunia 200 za mahindi.

Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.