“MNAPOPANGA MIPANGO ANGALIENI JITIHADA ZA JAMII” Beatrice Dominic
Mkurugenzi wa Manispaa Mtwara-Mikindani Beatrice Dominic amewataka Maafisa watendaji wa Kata na Mitaa kuzingatia jitihada za Wananchi wakati wa kupanga Mipango ya bajeti katika sehemu zao za kazi.
Amesema kuwa bajeti ya Halmashauri itategemea na mipango iliyopangwa kuanzia chini hasa miradi iliyoibuliwa na Wananchi.
Akizungumza katika Mafunzo ya Uhamasishaji jitihada za jamiikwa wtendaji wa Kata na Mitaa yaliyofanyika novemba 4,2017 kwenye ukumbi mdogo wa Chuo cha Ualimu Mtwara, Mkurugenzi wa manispaa alisema kuwa miradi yote ambayo jamii imefanya jitihada na kuchangia ipewe kipaumbele.
Ameongeza kuwa ana fahamu kuna miradi mingi katani imeibuliwa na ujenzi wake haujakamilika hivyo ni vema miradi hiyo ikikamilishwa.
“Miradi iliyofikiwa nusunusu ikamilishwe kwani haina haja ya kuanzisha miradi mipya wakati kuna miradi viporo”
Aidha amewataka watendaji hao kuhamasisha Wananchi kujitolea kwenye shughui mbalimbali za kijamii na kwamba mchango wao uwekwe kwenye bajeti ukipigia mahesabu kwenye kiwango cha pesa.
Vilevile amewasisitiza kuwa mipango iliyopangwa muda mrefu na haijatekelezwa ni vema mipango hiyo ikarudishwa kwa jamii kuona kama wanataka kuendelea nayo au la kwa kuwa mahitaji yanabadilika
Nae Kaimu Afisa mtendaji wa Kata ya Naliendele Hamisi Adam amesema kuwa changamoto kubwa inayowakuta ni kwamba Wananchi wengi hawapendi kuhudhuria mikutano na hivyo kupelekea mipango hiyo kupangwa na mtendaji pamoja na Mwenyekiti wa Mtaa na kupeleka kwenye kamati ya maendeleo ya Kata.
Amesema sababu kubwa inayopelekea Wananchi hao kutohudhuria vikao vya kuandaa mipango ni kwamba miradi mingi inayopitishwa kwenye mitaa ikifika kwenye ngazi ya halmashauri inakatwa na haitekelezwi na hakuna mrejesho hivyo inawapelekea wananchi kukata tamaa.
Manispaa Mtwara-Mikindani
Anuani ya Posta: P. o. Box 92,
Simu ya mezani: 023-2333102
Simu ya mkononi:
Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz
Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.