• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Mtwara-Mikindani Yatumia Mili.834.1 Kutekeleza Miradi ya Maendeleo

Posted on: January 10th, 2018

Jengo la Machinjio ya Chuno llililofanyiwa ukarabati na kuwa machinjio ya kisasa,hii ni sehemu ya ndani ya machinjio hayo

Katika kuhakikisha kuwa Manispaa Mtwara-Mikindani inaendelea kuboresha huduma za Jamii kwa Wananchi wake, imetoa na kutumia fedha kiasi cha shilingi milioni  834,074,361.79 kutoka katika mapato yake ya ndani Kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo, kuchangia mfuko wa Wanawake na Vijana pamoja na ulipaji fidia kwa wananchi.

Akizungumza Ofisini kwake mkurugenzi wa Manispaa Mtwara-Mikindani Bi Betarice Dominic amesema kuwa fedha ni mapato yatokanayo na kodi mbalimbali zinazolipwa na Wananchi na hivyo Manispaa imeona umuhimu wa kuzirudisha kwao ili kuimarisha miundombinu mbalimbali inayowagusa moja kwa moja.

Amesema kuwa Miradi iliyopelekewa fedha imegusa sekta mbalimbali zikiwemo sekta ya elimu, Utawala, Ufugaji na Uvuvi,Barabara,Afya pamoja na Kilimo. Aidha amewashukuru na kuwapongeza Wananchi  wa manispaa kwa kutekeleza wajibu wao wa kulipa kodi na kuwataka kuwa na utamaduni huo ili kuijenga Manispaa iliyo bora na yenye kuonekana.

Kwa upande wake Afisa Mipango wa Manispaa Ernest Mwongi amesema kuwa fedha zote zilizotolewa zimeshapelekwa kwenye Akaunti za miradi husika na kuna miradi mingine imeshatekelezwa na kukamilika, na miradi mingine  ipo kwenye hatua ya utekelezaji na kwamba  idara  ya mipango inahakikisha inaifuatilia kwa ukaribu miradi iliyobaki ili iweze kukamilika kwa wakati.

Ameitaja Miradi inayotekelezwa kulingana na fedha iliyotolewa ni pamoja na Mradi wa ujenzi  wa zahanati Mbawala chini, UKarabati wa Machinjio, Ujenzi wa matundu ya vyoo Shule ya Msingi Mbae na Mtawanya, Ujenzi wa Vyoo Shule za  Msingi Mjimwema, Shangani na Mlimani.

Miradi mingine ni Ujenzi wa Kalvati Miseti, Ununuzi wa pikipiki 5 kwa ajili ya watendaji wa Kata, Ununuzi wa gari la Mkurugenzi, Ujenzi wa Uzio  Ofisi kuu ya Manispaa, Ujenzi wa Shedi mwalo wa samaki Mirumba, Ununuzi wa gari la kufagia barabara pamoja na Ujenzi wa nyumba  za Wakuu wa Idara.

Fedha hizo vilevile zimeelekezwa katika Ujenzi wa Ofisi ya Kata Mtawanya na Tandika, Umaliziaji wa ujenzi Ofisi ya Kata Jangwani, Ujenzi wa choo soko la kiyangu, Ujenzi wa nyumba za walimu Namayanga, Ujenzi wa soko la Mitengo, Uandaaji na ununuzi wa miche ya Korosho, Ununuzi wa mbegu za Mtama, uwekaji wa nguzo na minyororo barabara ya TANU, Ujenzi wa vyumba vya madarasa 3 Shule ya Sekondari Mitengo na Mangamba, Pia Utengenezaji wa madawati na uwekaji wa Taa Stendi kuu ya mabasi.

Asha Mapesa mkazi wa Chuno amepongeza Manispaa kwa kazi wanayoifanya ya kuleta maendeleo na kuahidi kutoa ushirikiano kwenye kulinda rasilimali hizo kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.

Baada ya kufanya Mapitio ya bajeti 2017/2018 mwezi Desemba 2017, Manispaa Mtwara-Mikindani imepanga kukusanya bilioni 4,601,204,136 kutoka katika mapato yake ya ndani, Hadi Desemba 31,2017 Manispaa imekusanya bilioni 2,720,578,528 sawa na asilimia 59 ya bajeti iliyopangwa.



Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.