• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Mwalimu Nyange Apongezwa na Baraza la Wafanyakazi Kwa Kulipa Stahiki za Watumishi Mil.443

Posted on: December 12th, 2024

Wajumbe wa baraza la Wafanyakazi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani wamempongeza Mkurugenzi wa Manispaa  hiyo Mwalimu Hassani Nyange kwa kujali maslahi ya watumishi anaowaongoza na kuwalipa stahiki zao Shilingi 444,834,033 katika mwaka wa fedha wa 2023/2024.

Katibu wa Baraza la Wafanyakazi katika Manispaa hiyo  Justine Mkwara amesema kuwa ulipwaji wa stahiki hizo umeleta morali kwa watumishi kufanya kazi kwa kujituma na kuwataka wale ambao hawajalipwa stahiki zao kuwa na uvumilivu kwani malipo haya yanafanyika kwa awamu na kila mmoja atapata haki yake.

Nae Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara Ndugu Ashrafu Chusi ametoa pongezi kwa Mwalimu Nyange  kwa kuwalipa wafanyakazi stahiki zao na kuwa halmashauri pekee ndani ya Mkoa wa Mtwara inayokamilisha vikao vya baraza la wafanyakazi ambapo kupitia vikao hivyo watumishi wanapata nafasi ya kueleza changamoto zao.

“Manispaa ya Mtwara-Mikindani mmepata Mkurugenzi mzuri kuliko halmashauri yoyote ndani ya Mkoa huu, Sisi Vyama vya wafanyakazi tunajua utendaji kazi wa Wakurugenzi wote, Mpeni ushirikiano kama yeye anavyofanya, pendaneni na mumsaidie Mkurugenzi kwenye utendaji wake wa kazi kwa vitendo ili malengo ya halmashauri yatimie na tija ionekane”amesema Chusi

Kwa Upande wake  Mkurugenzi Nyange amesema kuwa pamoja na malipo ya stahiki mbalimbali,  halmashauri pia imekamilisha malipo ya walimu wa Idara ya Elimu ya Msingi na kwa sasa ataanza kulipa madeni ya walimu wa Sekondari Shilingi 145,000,000 ambapo ameshatoa Shilingi 52,000,000 kama malipo ya  awamu ya kwanza  na  yataanza kulipwa wiki inayofuata huku malipo ya madeni ya watumishi wengine yakifuata.

Aidha amewataka wajumbe wa baraza hilo kuhakikisha wanakusanya maoni, malalamiko, masononeko ya watumishi wanaowawakilisha na kuyafikisha  kwenye Menejimenti ili yafanyiwe kazi huku akiwasisitiza kuwapa elimu kuhusu maslahi yao ili kila mmoja atambue haki zake.


Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.