• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

RC Mtwara ammwagia sifa Mkurugenzi, ni katika utekelezaji wa Miradi

Posted on: June 26th, 2018


Baada ya kufanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya Maendeleo iliyotekelezwa kwa viwango vya juu  Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mhe Gelasius Gasper Byakanwa hakusita kutoa pongezi kwa Mkurugezi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani bi Beatrice Dominic kwa kuweza kutenga na kutumia fedha kutoka katika mapato ya ndani kwa ajili ya  utekelezaji wa miradi hiyo.

Pamoja na pongezi hizo amemtaka mkurugenzi kutoifanya jamii ya Manispaa kuwa tegemezi badala yake jamii hiyo ihamasishwe kuweka mikakati ya kuchangia kwenye elimu ikiwemo kuanzisha benki ya matofali yatakayosaidia kwenye ujenzi wa vyumba vya madarsa na nyumba za walimu.

Akizungumza kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyofabyika Juni 26,2018 Byakanwa amesema kuwa bado jamii ya Manispaa ipo nyuma kwenye uchangiaji wa shughuli mbalimbali hivyo amemtaka  mkurugenzi kutopeleka fedha  za ujenzi mahali popote hadi jamii ya sehemu husika iwe imechangia gharama ya ujenzi huo kwa asilimia 20.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewapongeza wananchi wa mbawala chini kwa kujitoa kwao kwenye ujenzi wa zahanati ya mbawala chini na kuwataka kuendelea kujitolea kwani maendeleo hayana ubaguzi wa aina yeyote

“Niwapongeze kwa kazi kubwa, niwapongeze kwa kutenga ardhi na kusafisha eneo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ni kazi kubwa na mnastahili pongezi, ninawaomba kwa pamoja tushirikiane kuleta maendeleo yetu maana Maendeleo hayana ubaguzi wowote”amesema Byakanwa

Aidha amemtaka Mkurugenzi kuwapa kipaumbele wafanyabiashara wadogo waliopo eneo la mkanaredi kwa sasa kwa  kuwapa maeneo ya kufanya biashara ndani ya stendi  ya muda ya Chipuputa  mara baada ya kukamilika na kuanza uendeshaji wake.

Pamoja na hayo Mkuu huyo wa Mkoa ametoa zawadi ya fedha kwa wanafunzi wa darasa la nne na saba wa shule ya Msingi Singino baada ya kuwauliza maswali na kuyajibu kwa ufasaha. Aidha ameahidi kuwashonea sare wanafunzi watano wa shule hiyo na kuwataka wazazi kuwajibika kuwanunulia sare watoto wao.

Sambamba na zawadi hizo kwa wanafunzi pia ameahidi kuwapatia Ofisi ya Kata ya Jangwani  meza na viti kwa ajili  ya matumizi ya Ofisi pamoja na bati 50 kwa zahanati ya mbawala chini  baada ya kuridhishwa na usimamizi mzuri uliofanyika kwenye majengo hayo..

Awali akiwasilisha miradi ya Maendeleo iliyosomwa mbele ya Mkuu wa Mkoa,  Mkurugenzi wa Manispaa Bi Beatrice Dominic amesema kuwa hadi kufikia Mei mwaka huu Manispaa imefikia asilimia 82 ya ukusanyaji wa mapato na  kutekeleza miradi Zaidi ya 47 iliyogharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.3.

Amesema kuwa Manispaa inaendelea kutii maagizo mbalimbali yanayotolewa na Serikali ikiwemo kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani katika kuchangia mfuko wa wanawake na vijana na kwamba hadi kufikia May mwaka huu Manispaa imetoa kiasi cha shilingi milioni 433  sawa na asilimia 100. Aidha Manispaa imetoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda kidogo cha ushonaji kitakachokusanya wajasiriamali Vijana na wanawake.

Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara inafanyika ikiwa ni muendelezo wa ziara yake iliyohusisha ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwenye halmashaurii zote zilizopo Mkoani Mtwara na M anispaa ya Mtwara-Mikindani ni halmashauri yake ya mwisho. Aidha ziara hii kwa Manispaa ya  imeanza tarehe 26 Juni na itaishia tarehe 27Juni 2018.  Ziara imehusisha ukaguzi wa miradi ya Maendeleo na usikilizaji wa kero mbalimbali za ardhi.





Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.