• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

RC Mtwara atoa wiki Tatu kwa TTCL kuhamisha Miundombinu

Posted on: November 1st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akikagua mradi wa mfereji mkubwa (km 3.4) wa kuondoa maji ya mvua kutoka skoya, Nabwada,shakur hadi Mtepwezi

Akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na Manispaa ya Mtwara-Mikindani kupitia  Mradi wa uendelezaji Miji Mkakati(Tanzania strategic Cities Project) na miradi ya TASAF Mkuu wa  Mkoa wa Mtwara Mhe.Gelasius Byakanwa ametoa wiki tatu  kwa  Kampuni ya simu ya TTCL kuhakikisha inaondoa miundombinu ya nyaya za mawasiliano zilizopo katika maeneo ya utekelezaji wa mradi

Agizo hilo limetolewa leo Novemba 1, 2018 baada ya Mhandisi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani Isaac Mpaki kulalamikia ucheleweshaji wa uondoaji wa miundombinu ya Kampuni hiyo katika maeneo ya mradi.

Amesema kuwa TTCL wameshalipwa fedha kiasi cha shilingi milioni 108 za kuhamisha miundombinu  tangu septemba mwaka huu lakini hadi kufikia sasa hakuna kilichofanyika.

Aidha Mhe. Mkuu wa Mkoa amezitaka Taasisi zote za Serikali kuwasiliana zinapotaka kutekeleza miradi ili kuepusha usumbufu.

"Ni vema Taasisi zote zinapotaka kutekeleza mradi zikawasiliana kabla mradi haujatekelezwa ili kuondoa gharama ambazo Manispaa imeingia katika kuhamisha Miundombinu "alisema Byakanwa

Pamoja na hayo Mhe Byakanwa amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa mradi kuongeza kasi na kuweka kipaumbele katika ujenzi wa mfereji mkubwa wa kuondoa maji ya mvua unaojengwa kutoka skoya kuelekea Nabwada hadi mtepwezi ili kuondokana na adha ya ujaaji wa maji katika  maeneo ikiwemo vifo na upotevu wa Mali.

Vilevile amewataka vijana waliopata ajira kwenye miradi hiyo kuwa waaminifu na kutokuhujumu miradi kwani ni faida ya Wanamtwara.

Byakanwa ameishukuru Serikali ya Tanzania na benki ya Dunia kwa kutenga fedha zilizolenga kuboresha miundombinu ndani ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani.

" Ninaamini baada ya kukamilika kwa Mradi huu Mtwara itakuwa sehemu nyingine na pengine tunaweza kupata sifa ya kuwa Jiji" alisema Byakanwa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani Kanali Emmanuel Mwaigobeko Amewataka wananchi wa Manispaa kulinda miundombinu inayojengwa na kama kuna mtu MTU yeyote anaoneka anataka kuhujumu mradi basi watoe taarifa mapema katika ofisi yake ili aweze kudhughulikiwa.

Mradi wa uendelezaji Miji   Mkakati inatekelezwa na Miji 8 iliyopo Tanzania na kwa Manispaa ya Mtwara-Mikindani ulianza kutelezwa tangu mwaka 2010 hadi sasa kupitia awamu mbalimbali. katika awamu hii ya pili mradi huu unajenga barabara zenye urefu wa km 4.2 Kwa kiwango cha lami, ujenzi wa mfereji mkuu wa kuondoa maji ya mvua wenye km 3.4 ujenzi wa sehemu za kupumzikia 3, ujenzi wa soko la  kisasa Chuno na ujenzi wa stendi ya mikindani ikigharimu fedha kiasi Cha Tsh.bilioni 21.7. Aidha wakandarasi wanaojenga mradi huu ni Kampuni ya M/S Jiangxi Geo-Engineering(Group) Corporation kutoka China.



Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.