• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Mikindani Municipal Council
Mtwara Mikindani Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Manispaa ya Mtwara Mikindani

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Idara ya Maji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi na Ugavi
        • Fursa za Uwekezaji
          • Vivutio vya Utalii
          • Maeneo ya Viwanda
      • Ufugaji wa nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
    • Muundo wa Kiutawala
    • Kata
      • Shangani
      • Rahaleo
      • Reli
      • Vigaeni
      • Majengo
      • Magomeni
      • Ufukoni
      • Mitengo
      • Magengeni
      • Mtonya
      • Kisungule
      • Jangwani
      • Mtawanya
      • Naliendele
      • Chikongola
      • Chuno
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • huduma za maji
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • HUduma za watumishi
    • Uzoaji wa taka ngumu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Ujenzi
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Kumuona Mstahiki Meya
  • Mradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi mipya
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba cha Picha

Mtwara-Mikindani yapitisha bajeti ya shilingi bilioni 39

Posted on: February 7th, 2019

Baraza la madiwani la Manispaa ya Mtwara-Mikindani limepitisha kwa aslimia mia moja rasimu ya bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 yenye jumla ya fedha kiasi cha shilingi yenye thamani ya shilingi bilioni 39,080,277,666 .

Akisoma taarifa ya mawasilisho ya mapendekezo hayo kwenye baraza la maalumu la madiwani la kupitia bajeti hiyo lililofanyika februari 7,2019 katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa hiyo, Mchumi wa Manispaa bwana Mensaria Mrema amesema kuwa katika makadiro hayo Manispaa imelenga kukusanya shilingi bilioni 4.9 kutoka katika mapato ya ndani, ruzuku ya matumizi ya kwaida milioni 658,ruzuuku ya mishahara bilioni 16.8na  miradi ya maendeleo bilioni 16.7

Amesema kuwa  mpango huu wa bajeti umelenga katika kuboresha maeneo mbalimbali ndani ya Manispaa kwa kuangalia vipaumbele vilivyogusa sekta mbalimbali zikiwemo Elimu, Afya na ustawi wa jamii, Maji na udhibiti wa maji taka, kilimo, mifugo na uvuvi, Majengo na miundombinu, Ardhi, misitu na maliasili, Maendeleo ya jamii, Utawala, Fedha na biashara.

Katika sekta ya elimu Manispaa imepanga kuboresha miundombinu ya shule za Msingi na Sekondari ikiwemo ujenzi wa madarasa, kujenga nyumba za walimu ,kujenga matundu ya vyoo, kuongeza udahili wa wanafunzi wa awali na darasa la kwanza ,ununuzi wa vifaa vya kufundishia, kuboresha mlo wa mchana kwa wanafunzi, kuongeza idadi ya walimu pamoja na kununua vifaa vya maabara.

Kwa upande wa sekta ya afya Mrema amesema kuwa Manispaa imelenga kupunguza vifo vya akina mama na Watoto pamoja na kuimarisha huduma na upatikanaji wa vifaa tiba kwa kuboresha miundombnu ya afya kwa kujenga zahanati mbili, kuimarisha upatikanaji wa vifaa tiba ,kusimamia matumizi ya mfumo wa Gothomis, kununua dawa na vitendanishi pamoja na kutenga  shilingi 1000 kwa kila mtoto kwa ajili ya lishe.

Sekta ya Maendeleo ya jamii manispaa imelenga kuwezesha wananchi kiuchumi kwa kutenga asilimia 10 katika mapato ya ndani kuwezesha vikundi vya wanawake,Vijana na walemavu, kutenga maeneo ya wajasiriamali na viwanda na upande wa utawala manispaa imelenga kuimarisha usalama ndani ya manispaa na kuboresha mazingira ya watumishi ya kufanyia kazi.

Sekta nyingine ni fedha na biashara ambapo manispaa imepanga kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya halmashauri kutoka 4.8 bilioni hadi 4.9 bilioni kwa kuongeza mashine za kukusanyia mapato pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato na kwa upande wa kilimo,mifugo na uvuvi manispaa imelenga kudhibiti uvuvi haramu ,kuongeza kasi ya uzalishaji mazao ya chakula na biashara, kuongeza thamani ya mazao pamoja na kuimarisha vyama vya ushirika.

Pamoja na hayo Mrema ameongeza kuwa katika kupanga bajeti hiyo manispaa imezingatia vigezo mbalimbali vikiwemo Mpango mkakati wa manispaa wa mwaka 2018/2019-2022/2023, wasifu wa halmashauri wa mwaka 2017, ilani ya uchaguzi ya Chama tawala ya mwaka 2015/2020, vipaumbele vya wananchi vilivyotokana na jitihada za jamii, sheria ya bajeti ya no. 11 ya 2015.

Vigezo vingine ni pamoja na mwongozo wa Serikali uliotolewa na wizara ya fedha mwaka 2018 juu ya maandalizi ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/2010, Malengo endelevu ya maendeleo ya umoja wa mataifa ya mwaka 2016, Maagizo na ahadi za viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na mapitio ya mpango wa maendeleo wa mwaka 2018/2018.

Katika mwaka wa fedha wa 2018/2019 Manispaa ilipanga kukusanya fedha kaisi cha shilingi bilioni 29,144,145,260 kutoka katika vyanzo mbalimbali , kufikia Disemba 2018 Manispaa imeshakusanya fedha kiasi  cha shilingi bilioni 14,123,869,490.51 (mapato ya ndani bilioni 1.368,584,953.70 sawa na asilimia 29), (Misharaha 6,379,030,000 sawa na asilima 44), (Matumizi mengineyo shilingi 338,622,427 sawa na asilimia 50), (Miradi ya Maendeleo 6,037,632,109.8 sawa na asilimia 134.

Matangazo

  • Taarifa Kwa Umma ya Ilani ya Kuondoka Kwenye Kiwanja Nmaba 1-149 Litingi January 03, 2025
  • Taarifa Kwa Umma Ufafanuzi Kuhusu Jina la Shule ya Sekondari Mwalimu Nyange January 02, 2025
  • Terms Of Reference For The Provisions Of Construction Supervision Consultancy Services For Urban Infrastructures Development In Mtwara Mikindani Municipality Under The TACTIC Project March 07, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili Nafasi ya Mwandikishaji Msaidizi na BVR Operators January 09, 2025
  • Tazama yote

Habari mpya

  • Kamati ya Siasa Mkoa Yapongeza Utekeelzaji wa Miradi ya MaendeleoMtwara-Mikindani

    January 08, 2025
  • MD Nyange Ateta na Watumishi Wa Kada ya Afya

    January 07, 2025
  • Vikundi Vilivyopata Mkopo Vyahimizwa Kurejesha Fedha Kwa Wakati

    January 06, 2025
  • Mtwara-Mikindani Yatoa Mkopo wa Mil.640.9 Kwa Vikundi 58

    January 06, 2025
  • Tazama yote

Video

Namna ya Kujisajili na Kutumia mfumo wa Uhamisho kwa watumishi wa Umma
Video nyinginezo

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni ya ujenzi wa barabara km 4.1,Ujenzi wa Mfereji wa maji ya mvua toka Skoya,nabwada hadi Mtepwezi,Ujenzi wa soko la Chuno,Ukarabati wa stendi ya Mikindani pamoja na Uboreshaji wa sehemu za kupumzikia na michezo
  • Kupata matokeo ya Darasa la nne 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Matokeo ya Kidato cha Pili 2017 Manispaa Mtwara-Mikindani
  • Taratibu za Kupata fomu za Vileo

Viunganishi linganifu

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • OR - TAMISEMI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Manispaa Mtwara-Mikindani

    Anuani ya Posta: P. o. Box 92,

    Simu ya mezani: 023-2333102

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@mtwaramikindanimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018Mtwara Mikindani Manispaa . All rights reserved.